BORA NIENDE(17)
KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com
ILIPO ISHIA....
JACK nawasili
buguruni alipo mdogo wake huyo Melissa
Jack nafika nakutana
na mshichana mrembo Sheila.
Namkamata mkono
wakati wa salamu nabakia kumng'ang'ania.
Naingia ndani napo
Melisa ananieleza vitu nisivyo vielewa yani nabakia njia panda.
Huku akisema wiki hii
anataka kumfanyia kitu mtu ampendae.
SONGA NAYO..........
"Kaka utanielewa
tu, maana hii siku niliitamani sana ya kukutana na wewe na kukuambia wewe kaka
yangu na kukurambulisha kwa mtu niliyotokea kumpenda sasa japo sikuwahi
kufikiria kama nitapenda.
Lakini hata kama
ananipenda bado sipo tayari kumvulia nguo yangu hii mpaka pale nitakapo funga nae
pingu za maisha aniite mke na mimi nimuite mume.
Hapo ndipo nitafanya
mapenzi kwa mara ya kwanza"
Aliongea Melisa na
kunifanya gafla nibadilike na kufura hasira huku nikiwa natetemeka mpaka
kushindwa kuongea na kubaki nikimtizama tu.
Jinsi alivyokuwa akiongea.
"Kweli
umenichoka na ni bora ungeniambia mapema nikajua ili nisije au nije sikutegemea
kama nakuja kuutesa moyo wangu.
Melisa kweli
nilishindwa kuvumilia lakini sasa ndiyo umeniuwa kabisa, sikutaka kukufosi
maana upendo haulazimishi lakini pia jithidi uliyempata awe na mapenzi ya dhati
maana vijna wengi hawaaminiki sasa wamegeuza mapenzi kama mchezo na hawajui
wanacheza na hisia za mtu"
Niliongea huku nikia
siamini kunachonitokea , kama kweli Melissa ninae mjua mimi amepata mpenzi na
leo au yani mchana wake pakikucha ananitambulisha.
Roho ilikuwa ikiuma
sana mpaka najikuta natetemeka na meno yanagongana ya chini na ya juu.
"Hapana kaka
usilie basi nakupenda wewe kaka yangu, na nimekuita ili tu uje nikuambie kama
nakupenda na nipo tayari kuishi na wewe, hivyo nakuahidi kuanzia sasa nitakuwa
na wewe na nitaishi na wewe nakupenda sana.
Na wewe utakuwa ndiye
mume
wangu huku upande
mwingine ukisimama kaka yangu.
Na sinta kusaliti
nakuahidi nikikusaliti kichwa changu chinjia chini au nipe adhabu yoyote
uipendayo narudia kukuahidi tena".
Aliongea Melissa na
kunifanya nibaki nikishangaa nikiwa siamini maneno anayo yaongea Melisa .
Ili kuamini kama
nikweli anachokiongea melisa alinikumbatia kisha kunitizama na kunitamkia.
"Nakupenda na
nirazidi kukupenda"
Nilimtazama bila
kupata jibu na kuamua kumvuta kifuani kwangu na kuanza kuunyonya mdomo wake
uliokuwa mlaini.
Kila jitu nilichokifa
Melissa alikua mgeni hata denda akuwa hakifahamu kupiga zaidi tu aliniachia
kila kitu nifanye mimi.
Baada ya kumshika
melisa kidogo nilimuona ni mtu mwenye joto kali la hisia hivyo ilinibidi
nimuache tu maana pale niliingia kama kaka hivyo ningefnya kitu tayari
ningemfanya Melisa anatabia mbaya.
Nilivumilia na
kuepusha lawama nilimuomba niondoke lakini alikataa na kuniambia yeye ataenda
kulala kwa eafiki yake kama naogopa kulala naye na hatimaye aliondoka na mimi
nikafunga mlango nikalala.
Asubuhi nilikua
wakwanza kumwamsha ili niondoke kuwahi kufungasha vitu vya dukani nilimpatia
pesa ya matumizi na kuondoka zangu huku moyoni nikiwa na kila aina ya furaha
kwani hiyo ilikuwa ni furaha kubwa sana kumpata Melisa.
"Hello Jackson
natumaini ni mzima tena wa afya na naimai unanijua vizuri mimi n nani.
Mimi ndiye Mr David
tajiri mwenye pesa zangu na ninauwezo wa kufanya chochote bila hata kushindwa
na nauwezo wa kugeuza ukweli kuwa uongo hivyo baada ya kusoma ujumbe huu
nitafute kwa faida yako kabla sijakutafuta mimi"
Ni meseji iliyokuwa
nimetumiwa na boss wangu aliye nizulumu nyumba na kunifanya niishi nyumba ya
kupanga.
"Wewe niache tu
uliyo nifanyia yananitosha lakini bado unanisumbua au unaitaka roho yangu sema
tu mimi nije uniuwe na siyo kunipiga mikwara kila siku nimekuchoka Mr
David"
Nilimjibu kwa
kumuandikia meseji kama alivyo tuma yeye na mimi kuendelea na kazi zangu za
kuandika bizaa zilizoisha ili niiende duka la jumla kuongeza vitu vilivyo isha.
"Andika haraka
haraka leo nafuraha sana dogo hivyo sema na wewe nikuletee zawadi gani yani
namaanisha yoyote uipendayo , na leo nikirudi tu wewe leo ni off yako yani
uzurure mpaka saa mbili urudi maana leo nipo na furaha sana"
Niliongea huku
nikiendelea kutaja vitu vilivyo isha.
Na hatimaye nilianza
safari ya kuelekea soko la tandika kukusanya mzigo wa dukani.
Taratibu nikiwa na
kipikipiki changu kidogo nakatika mitaa huku nikiwa na fura ya ajabu kuwahi
kutokea,
Furaha niliyo kuwa
nayo ilinifanya hata matatizo niliyo nayo niyasahau kisa tu nimempata Melissa
msichana niliyempenda na kumjali kwa kila hali .
Na kumuona yeye ndiye
kila kitu kwangu na kama ningemkosa basi ningejihisi ni mwenye mkosi katika
maisha yangu .
"Kipindindi
nikiwa na pesa wengi sana walinipenda lakini niliwakwepa ili nimalize ujenzi wa
nyumba yangu, na baada ya nyuma kuisha hata miezi sita sijamaliza ijapigwa
mnada.
Bora hata pesa zangu
ningezitumia kula bata na warembo waliokuwa wakinitaka kupindi kile na mimi
kuwakataa.
Leo niingekuwa hivi
mimi natembea na pikipiki"
Niliwaza sana wakati
nazidi kuvuta mafuta katika pikipiki yangu ya mzigo.
Baada ya kufika
Tazara nimeshaanza kuikamata barabara ya Temeke nilishtuka na mlio mkali wa oni
uliopigia nyuma ya pikipiki yangu.
"Piiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii"
Honi ilipigwa bila
hata kuachiwa zaidi mpigaji aliendelea kuibonyeza na gafla simu ikaita kucheki
ni namba ya Mr David.
"Naomba tukutane
Temeke kituo cha usalama katika stendi ya daladala.
Sasa hivi nimekuona
hapo na mimi ndiyo niliokupigia honi nazani umenielewa kuna kitu nataka
kukuambia"
Aliongea baada ya
kupokea simu na alipo maliza alikata bila kunipa nafasi ya kuongea mimi.
ITAENDELEA...................
No comments:
Post a Comment