BORA NIENDE(16)
KING SOKA
PHONE:+255717758864
DAR ES SALAAM_TZ
PAGE
#STORY_ZA_KING_SOKA
Email address
jacksonsoka@gmail.com
Sehemu ya kumi na
sita iliishia pale nilipo pokea simu kwa mtu nisiye mfahamu na kujitambulisha
yeye ni boss wangu.
Nilibaki nimebutwaa
huku nikimuuliza boss wangu akajibu ndiyo
Tuliishia hapo
SONGA
NAYO.................
"Ndiyo mimi ni
boss wako.
Inamaa umenisahau
boss wako kisa kukufunga na kukufilisi.
Hahahahahaha! Kijana
wewe ni mjinga sana na utakufa masikini, na sisi wenye pesa tutaendelea kula
raha za dunia mpaka siku ya kufa na wewe kulia masikini mpaka siku ya
kufa"
Aliongea boss wangu
na kunifanya nibaki mdomo masikio vyote vikiwa vimepatwa na bumbuwazi.
Kwa maneno aliyoyatoa
boss wangu huyo aliysnianya mpaka leo nikiwa naishi nyumba za kupanga kitu
ambacho sikuwahi kufikiria katika maisha yangu.
Hakuishia hapo tu
bado aluzidi kuongea maneno mengi ya kejeli na zarau.
"Jackson kijana
mdogo uliyeingia katika matatizo makubwa ambayo utaweza kuyamaliza kirahisi.
Nakusikitia sana mtu
kama uliyekuwa na nyumba nzuri gari na mali za kutosha leo umekuwa kama mbwa wa
muokota mifupa"
Aliongea boss wangu
akizidi kunikejeli kwa maneno yakunitisha tamaa na kejeli ndani yake.
"Uliku boss
wangu zamanu lakini sasa wewe ni binadamu kama binadamu wengine, wewe ni tajiri
mimi masikini lakini wote tutaenda chini.
Sikupenda yanitokee
yalio nikuta lakini yalisha tokea na sasa naanza upya nyumba yangu imeuzwa
chanzo wewe kunisingizia mwizi kwa kitu nisicho husika sasa unazani mimi nitakusamehe
vipi katika maisha yangu, mimi nakuchukia kwa kurudisha maisha yangu nyuma tu,
na siyo kwa kingine.
Sasa mimi ni masikini
tu na sijui lini nitajenga lakini lazima nitajenga, hivyo usinikejeli sana ni
moja ya msisha niliyo andikiwa na Mungu.
Jela nimekaa gari
yangu umechukua ,nyumba umeuza, lakini vyote ni mali yangu halali lakini
kwakuwa wewe pesa unazo unafanya uwezavyo.
Na bado ukurizika
sasa umeanza kutaka kuitoa roho yangu kabisa wewe usijali nipo tayari kufa kama
ikibidi lakini siyo kwa uwezo wako labda uwezo wa Mungu na Mungu akitaka
nife"
Nilimjibu kwa hasira
mpaka kila aliyekuwa akipita njiani karibu na duka kusimama na kunisikiliza kwa
makini huku watu waliokuja dukani nao walibaki kunishangaa.
Boss wangu huyo
akuishia hapo bado alinitukana sana katika simu na sikutaka kukata simu ili
nifahamu mengi zaidi kuhusu chanzo cha mimi mpaks nyumba yangu iuwezwe kisa
kilikuwa nini.
Nilitamani sana
kufahamu chanzo lakini alikata simu na kuniacha njia panda nikijiuliza ni kwa
nini amenipigia siku na kunisema kihasi hiki uku akinicheka sana mpaka nilipata
hasira.
"Kaka leo nina
zawadi nzuri nataka kukupa hivyo ningependa uje huku buguruni leo, ikiwezekana
hata kulala utala uku kama ukikosa gari ya kurejea nyumbani, mimi nitalala
katika kochi na wewe kitandani.
Niahidi basi kama
utakuja yani usichelewe maana ni zawadi nzuri sana msishani mwako na
utaifurahiya sana naimani"
Mesagi ya Melisa
iliingia katika simu yangu na kunifanya nibaki nikishangaa niende buguruni saa
tatu tena ikiwezekana tulale nae chumba kimoja je nikimbaka itakuaje.
Nilitulia kimya kwa
muda kisha nikakubalina na Melisa kwa kumjibu mesegi yake kama naenda hivyo
aondoe shaka.
Mda mfupi badae
niliianza safari ya kuelekea buguruni, huku nyumba nikimuacha kijana aliyekuwa
ndiye ananisaidia kuuza duka kwani alikua akilala humo humo ndani nilimpsngia
chumba cha kuishi kama yeye, na mimi nikaelekea kupanda gari na safari ikianza.
Hatimaye nilifika
buguruni sheli na kushuka .
Na kuanza kurudi kama
narimudi vingunguti kuelekea nyumbani kwa Melisa.
Niliwasili ikiwa ni
tayari majira ya saa nne na dakika hamsini na sita usiku(23:56 usiku)
"Waooooh kaka
umefika!
Ujue siamini kama ni
wewe kweli"
Alinipokea Melisa.
Kwa kunirukia na
kubembea na shingo yangu mpaka wapangaji wenzake waliokuwa bado wapo njee
walishangaa kwa jinsi alivyo nirukia kwa furaha.
"Nimefika
namshukuru Mungu kidogo nilipotea lakini nimefika ni jambo la kushukuru"
Niliongea mimi baada
ya kuwa nimesha wasili nyumbani kwa Melisa na kumkuta njee amekaa na baazi ya
wapangaji wenzake.
"Jamani huyu ni
kaka yangu anaitwa Jackson.
Anaishi airport
karakata.
Kaka huyu ni Mama
Abdul, yule Sheila, huyu mama Issa,na huyo Dada Zakia"
Alinitambulisha
Melisa kwa wapangaji wenzake aliokuwa nao njee.
"Namshukuru
kuwafahamu pia nashukuru kwa kuishi vizuri na Melissa"
Niliongea huku
nikiwasalimia kwa kuwashika mkono.
Nilipofika kwa Sheila
ilinibidi nigande kwanza kisha nimuangalie usoni maana.
Mtoto alikua
ameumbika akaumbika uzuri wa sura upombo mpaka mavasi, tatizo sikuweza kutambua
tabia yake tu.
Nilibaki
nimeushikilia mkono wa Sheila bila hata kumuachia huku nikiwa namtazama mara
mbili kama siamini kwa ninacho kiona kutokana na uzuri wake alio jaaliwa na
mwenyezi Mungu.
"We Kaka!"
Nilishuka baada ya kusikia
sauti ikisema we Kaka ndipo nastuka kumbe nimekumbatia mkono wa mtu.
"Samahani Dada
nilijisahau unajua leo nipo na furaha sana kukurana na Melisa.
Ndiyo maana"
Niliongea mimi kwa
aibu sana uku nikiangalia chini.
"Kaka ujue mimi
sina zawadi yoyote ninayo taka kukupa zaidi ya hiki ninachotaka kukuambia Kaka
yangu.
Kaka nasikitika
kukuambia kama naona undugu unaenda kupotea vile"
Aliongea Melisa kwa
sauti ya utaratibu misili ya mtu anaetaka kulia.
"Kwa nini!
umesema hivyo Melissa kwani tatizo nini?"
Nilimuuliza Melissa
"Kaka mimi
nimeona niolewe tu na atakaye niowa nimesha mpata na kaniahidi kila kitu kizuri
na maisha mazuri.
Na pia mpaka leo bado
ajafanya kitu chochote mwilini mwangu.
Lakini kwa wika hii
nataka nifanye kitu juu yake"
Aliongea Melissa huku
akiwa anaangalia chini
"Unasemaje
Melissa mbona kama sikuelewi vile"
Niliongea kwa ukali
nahisi mpaka waliokuwa njee walisikia.
ITAENDELEA...................
No comments:
Post a Comment